Meneja Mawasiliano wa shirika la Tanesco Bi.Badra Masoud akiongea na waandishi wa habari juu ya mkutano wa Mawaziri wa Nishati wa Nchi za Afrika Mashariki na Kati mwa Afrika unaotarajiwa kuanza (leo) jijini Arusha ambapo Tanzania itakuwa mwenyeji wa mkutano huo
Tanzania imebahatika kuwa mwenyeji wa mkutano(5) wa mawaziri wanaosimamia Nishati ya Umeme kutoka nchi 11 zilizo Mashariki na Kati mwa Afrika wanaounda mtandao wa nishati na umeme maarufu kama”East Afrika Power Pool (EAPP) unaotarajiwa kuanza rasmi leo jijini Arusha
Hayo yamesemwa na Afisa uhusiano wa shirika la umeme (TANESCO) Bi.Badra Masoud wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya mkutano huo mkubwa ambao unatarajiwa kufanyika jijini hapa
Bi.Masoud alisema kuwa Tanzania ni mwanachama wa mtandao wa (EAPP) ulionzishwa miaka 6 iliyopita ikiwa na lengo la kurahisisha upitakanaji wa nishati ya uhakika ya umeme kwa nchi wanachama wa EAPP kwa kujenga njia kuu ya kusafirishia umeme unaounganisha nchi hizi.
Alifafanua kuwa Tanzania inahitaji kuboresha maisha ya wananchi wake katika Nyanja nyingi kama vile matibabu,elimu,upatikanaji wa maji safi na salama,uzalishaji,Ongezeka la viwanda na kurahisisha matumizi ya majumbani.
Alisema kuwa haya yote yatawezekana tu kama kutakuwa na umeme wa uhakika na wenye gharama nafuu ili wananchi waweze kumudu gharama hizo bila matatizo yeyote.
Bi.Masoud alisema ili kupata umeme wa uhakika na gharama nafuu,Mawaziri wa nchi hizi 11 watatoka na mwongozo wa utekelezaji wa kuunganisha miundombinu ya njia kuu ya kusafirisha umeme kwenye nchi za Afrika Mashariki na Kati mwa Afrika.
“kwa sasa tunanunua umeme bei ghali sana kutoka kwa wazalishaji binafsi (Independent Power Producer-IPP) ambao wanatuuzia umeme kwa bei ghali sana hivyo TANESCO inaponunua umeme kwa bei ghali sana na kuiuza kwa bei kawaida inaipelekea kupata hasara na hata kupandisha bei ili kukidhi gharama za uendeshaji.”alisema Badra
Wanahabari wakiwa kazini
Hata hivyo alisema kuwa mkutano huo utatanguliwa na Wakurugenzi wa mashirika yaliyo na dhamana ya kuzalisha,kusafirisha na kusambaza umeme,wakiwepo wadau wa Mamlaka za Udhibiti wa Nishati ya Umeme wataanza mkutano wa awali utakaofuatiwa na mkutano wa Mawaziri siku ya Jumamosi.
Alisema kuwa nchi wanachama wa EAPP,ni Tanzania ,Kenya,Uganda,Ethiopia,Rwanda,Burundi,Libya,Egypt,Republic of Sudan,Demokratic Republic of Congo(DRC) na Djbouti.